Yanga SC

MZUNGUKO WA PILI MAMBO YALIKUWA MAGUMU KWA KAZE, CHEKI REKODI ZAKE

admin March 8, 2021 9:47 am


MZUNGUKO wa pili, Kocha Mkuu wa Yanga, Cedric Kaze mambo yalikuwa magumu kwake kutokana na kushindwa kupata matokeo chanya kwenye mechi zake 6 za Ligi Kuu Bara aliweza kushinda mechi moja.

Ndani ya dakika 540 alipokuwa akisaka pointi 18 aliambulia jumla ya pointi 7 na kuangusha pointi 11. 

Alishinda mchezo mmoja, alipoteza mchezo mmoja na kukusanya jumla ya sare nne ambazo zilimpa pointi nne na kumfanya jumla awe na pointi 7 ndani ya uwanja katika mechi 6.

Alianza sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Tanzania Prisons, Mbeya City 1-1 Yanga, Yanga 3-3 Kagera Sugar na alishinda mbele ya Mtibwa Sugar bao 1-0.

Kichapo ilikuwa mbele ya Coastal Union kwa kichapo cha mabao 2-1 na mchezo wake wa mwisho ilikuwa mbele ya Polisi Tanzania kwenye sare ya kufungana bao 1-1, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Jana Machi 7, yeye pamoja na benchi lake la ufundi wamefutwa kazi jumlajumla.

SIMBA vs PRISONS UWANJA WA MKAPA NI VITA YA KISASI BUSWITA: HATUKUWA NA CHA KUPOTEZA NDANI YA UWANJA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply