Taifa Stars

STARS YAPAA KUWAFUATA KENYA, KASEJA AAHIDI MAKUBWA

admin March 13, 2021 3:47 pm


KIKOSI cha Taifa Stars kimeanza safari ya kuelekea nchini kwa ajili ya michezo miwili ya kujipima nguvu dhidi ya kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya.

Stars inataka kuitumia michezo hiyo hiyo ambayo inatarajiwa kupigwa Machi 15, na 18 mwaka huu kama sehenu ya maandalizi ya michezo ya kusaka tiketi ya michezo ya kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika (AFCON), dhidi ya Equatorial Guinea na Libya.

Stars chini ya kocha, Kim Poulsen ilianza kambi rasmi siku ya Jumatatu iliyopita katika uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Akizungumzia maandalizi yao mchezaji Mwandamizi, Juma Kaseja amesema: “Kikosi kimekuwa na wasaa mzuri wa mazoezi ya kujiandaa na michezo yetu dhidi ya Kenya na ile ya kutafuta tiketi ya kufuzu AFCON.

“Tunajua mbele ya Kenya haitakuwa michezo rahisi kutokana na ukweli kwamba tunajuana vizuri, lakini kutokana na ari niliyoiona kwa wachezaji naamini tutafanya kitu kizuri,”

IDD NADO AMEWAKA HATARI MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA JUMAPILI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply