Simba SC

SIMBA YAMTAJA MBADALA WA MORRISON

admin April 21, 2021 10:47 am

 


WAKATI leo Uwanja wa Kaitaba, Didier Gomes, Kocha Mkuu wa Simba akitarajiwa kuikosa huduma ya kiungo mchetuaji, Bernard Morrison amemtaja mchezaji ambaye atachukua mikoba yake.

Gomes raia wa Ufaransa amesema kuwa atamkosa Morrison kutokana na kukusanya jumla ya kadi tatu za njano ambazo alizipata kwenye michezo mitatu tofauti.

Mfaransa huyo amesema:”Nitamkosa Morrison, (Bernard) kwa kuwa ana kadi tatu za njano ambazo alizipata hivyo kukosekana kwake kumevuruga mipango ya timu.

“Ila kwa kuwa yeye nitamkosa basi nina amini kwamba yupo Luis (Miquissone) anaweza kucheza kwenye nafasi yake hiyo na yupo fiti kwani mchezo uliopita alipumzika jambo ambalo linamaanisha kwamba atafanya majukumu yake vizuri,” .

MITAMBO MIWILI YA KAZI AZAM YAREJEA KUNDINI, KUIWAHI YANGA VIDEO: YANGA YAITAKA SIMBA KWA MKAPA, YATAMBA KUSEPA NA UBINGWA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply