Yanga SC

MAENDELEO YA KISINDA NA DICKSON JOB YALETA MATUMAINI YANGA

admin April 22, 2021 1:47 pm


 NYOTA wawili wa kikosi cha Yanga, ambao walipata maumivu kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Gwambina FC kwa sasa hali zao zinaendelea vizuri jambo ambalo linaleta matumaini kwa nyota hao kurejea kwenye majukumu yao.

Job ambaye ni beki ikiwa ni mchezo wake wa pili kucheza ndani ya Yanga akitokea Mtibwa Sugar alipata tatizo la maumivu ya misuli ya nyama za paja jambo lililomlazimu kuomba mabadiliko na nafasi yake kuchukuliwa na Bakari Mwamnyeto.

Mchezo wa kwanza wa Job ilikuwa Yanga 1-0 Biashara United na mchezo wa pili ambao hakuyeyusha dakika zote 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Yanga 3-1 Gwambina FC.

Mwingine ni Tuisila Kisinda ambaye alipata maumivu ya bega yeye nafasi yake ilichukuliwa na kiungo Said Ntibanzokiza.

Taarifa rasmi iliyotolewa na Yanga imeeleza kuwa nyota hao wanaendelea vizuri kwa sasa.

SIMBA YAGOMEA UBINGWA WAO KWENDA YANGA, HESABU ZAO HIZI HAPA KMC WAFUNGUKIA KUHUSU UBINGWA WA LIGI KUU BARA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply