Yanga SC

YANGA: MCHEZO MKUBWA HUCHEZWA NA WACHEZAJI WAKUBWA

admin May 7, 2021 2:47 pm


HARUNA Niyonzima, kiungo mchezeshaji wa Klabu ya Yanga amesema kuwa mchezo mkubwa huchezwa na wachezaji wakubwa hivyo wao hawana mashaka kuelekea mchezo wa kesho.

Kesho, Mei 8, Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Nassreddine Nabi ina kibarua cha kusaka pointi tatu muhimu mbele ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes. 

Walipokutana Novemba 7 ndani ya Ligi Kuu Bara,  ubao ulisoma Yanga 1-1 Simba hivyo kesho ni mchezo wa kukata na shoka. 

“Mchezo mkubwa huchezwa na wachezaji wakubwa hivyo hatuna mashaka kuhusu mchezo wetu wa kesho tupo tayari na tutapambana,” .



MO AWAPIGIA SIMU WACHEZAJI WOTE SIMBA SC SIMBA: TUMEJIPANGA KUPATA USHINDI MBELE YA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply