epl

KANE AWAOMBA MABOSI WAPOKEE OFA

admin May 10, 2021 7:47 pm


HARRY Kane, mshambuliaji wa kikosi cha Tottenham amemwambia mmiliki wa timu hiyo Daniel Levy apokee ofa ambazo zimekuwa zikimuhitaji.

Klabu mbalimbali zimekuwa zikikihitaji saini ya nyota huyo ili ziweze kupata huduma yake kwa ajili ya kuzitumikia kwa msimu ujao.

Miongoni mwa timu ambazo zimepeleka ofa ya kumpata nyota huyo ni pamoja na Manchester United ambayo iliweka dau la pauni milioni 90 kwa ajili ya kumpata mshambuliaji huyo.

Imekuwa ikieelezwa kuwa Kane amewaambia mabosi wake kwamba anataka kuondoka ndani ya Spurs ili kwenda kujiunga kwenye timu inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

Kichapo cha mabao 3-1 walichokipata Spurs na Leeds juzi kimepunguza matumaini kwa timu hiyo kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao na alijiunga na timu hiyo mwaka 2004.

VIDEO: SIMBA QUEENS WAPEWA ZAWADI YA GARI JIPYA DUH! KUMBE SIMBA WANATAKA YANGA ISHUSHWE MADARAJA MAWILI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply