Ligi Kuu

KMC KAMILI GADO KUIVAA AZAM FC

admin May 12, 2021 1:47 pm

 CHRISTINA  Mwagala, Ofisa Habari wa Klabu ya KMC amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC. 

KMC inakumbuka kwamba imetoka kulazimisha sare ya bila kufungana na Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara walipokutana Uwanja wa Majaliwa.

Azam FC wao mchezo wao wa mwisho wa ligi walikamilisha kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga, Uwanja wa Mkapa na kusepa na pointi tatu mazima. 

Walipokutana mzunguko wa kwanza,  Uwanja wa Uhuru, ubao ulisoma KMC 1-0 Azam FC na kuwafanya Azam FC kuyeyusha pointi tatu jumlajumla. 

Mwagala amesema:”Tunahitaji kuwaoyesha Azam FC kwamba hatukufanya makusudi kuyeyusha Ice Cream katika mchezo uliopita, tupo imara na tunakwenda Azam Complex tukijiamini,” .

KAMATI YA MASAA 72 YATOA TAARIFA KUHUSU SIMBA V YANGA SIMBA YATAKA KUSEPA NA MAKOMBE YOTE BONGO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply