Azam FC

AZAM FC V KMC NI SAA 1:00 USIKU, MUDA WABADILISHWA

admin May 15, 2021 6:47 am


MCHEZO wa Ligi Kuu Bara kati ya Azam FC dhidi ya KMC utachezwa saa 1:00 usiku badala ya saa 10:00 jioni.


Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa KMC, Christina Mwagala amesema kuwa muda wa mchezo huo umebadilishwa tofauti na awali.

Mwagala amesema:”Mechi yetu ya KMC dhidi ya Azam FC umebadilishwa muda kutoka saa 16:00, (10:00) jioni tena ni saa 19:00, (1:00) usiku, Uwanja wa Chamazi. Nawatakia sikukuu njema,”.

Mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Uhuru, ubao ulisoma KMC 1-0 Azam FC hivyo leo utakuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili kusaka pointi tatu.
Kwenye msimamo KMC ipo nafasi ya 5 na pointi zake 41 inakutana na Azam FC iliyo nafasi ya tatu na pointi 54,
SIMBA WATAMBA KUPATA USHINDI MBELE YA KAIZER CHIEFS LEO, KOCHA WA REAL MADRID ZIDANE KUTIMKA MAZIMA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply