Yanga SC

KOCHA NABI WA YANGA ATOA MAAGIZO MAALUMU

admin May 30, 2021 9:48 am


 NASREDINE Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga amewaambia wachezaji wake kuwa wanahitaji kutwaa mataji mawili kwa msimu huu wa 2020/21 ili kufikia malengo ambayo walianza nayo mwanzo wa msimu.


Mataji hayo ni pamoja na Kombe la Shirikisho ambapo tayari Yanga imetinga hatua ya nusu fainali baada ya ubao wa Uwanja wa Kambarage, Shinyanga kusoma Mwadui 0-2 Yanga hivyo inatarajiwa kucheza na Biashara United hatua ya nusu fainali.


Kwenye upande wa ligi ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 61 baada ya kucheza mechi 29 na ina mechi  tano mkononi kukamilisha mzungukuko wa pili.


Kwa mujibu wa Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz alisema kuwa kocha huyo raia wa Tunisia aliongea na wachezaji na kuwaambia kwamba bado wana kazi ya kufanya kutimiza malengo.


“Nabi ameongea na wachezaji na kuwaambia kwamba bado kazi inaendelea na anahitaji kuona wanafanikisha lengo la kufanya vizuri kwenye Kombe la Shirikisho pamoja na ligi kwani bado mapambano yanaendelea na kazi itaendelea mpaka mwisho,” alisema Nugaz.


Makombe yote mawili ambayo wanapigia hesabu Yanga yapo mikononi mwa watani zao wa jadi Simba ambao nao walibainisha kwamba wanahitaji mataji yao.

KUSHUKA DARAJA NI SUALA LISILOEPUKIKA MUHIMU KUJIPANGA KAIZER CHIEFS WAMTAKA GOMES KUVAA VIATU VYA HUNT

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply