Yanga SC

MUKOKO WA YANGA ANASAKWA NA VIGOGO AFRIKA

admin May 30, 2021 4:48 pm


UONGOZI wa kikosi cha klabu ya Yanga umekiri kuwa Mkata umeme wao Mkongomani, Mukoko Tonombe anazivutia klabu nyingi kubwa barani Afrika, ambazo zimeonekana kuhitaji huduma ya mchezaji huyo.

Mukoko ambaye amebakisha mwaka mmoja tu katika mkataba wake na klabu ya Yanga ameonekana kuzivutia baadhi ya klabu kubwa wakiwemo wababe wa soka kutokea nchini Guinea, Horoya ambao wanatajwa kuweka dau la zaidi ya Shilingi Milioni 400 za Kitanzania kwa ajili ya kupata huduma yake.

Mukoko akiwa katika msimu wake wa kwanza tu ndani ya kikosi cha klabu ya Yanga, amefanikiwa kuhusika katika mabao nane akifunga mabao manne na kuasisti mabao manne mpaka sasa.

Akizungumzia ishu ya dili la Mukoko, Mkurugenzi wa mashindano wa klabu ya Yanga, Thabit Kandoro amesema: “Ni kweli zimekuwepo baadhi ya timu kubwa barani Afrika, ambazo zimeonyesha nia ya kuhitaji saini ya kiungo mkabaji wetu Mukoko Tonombe.

“Hii inatokana na ukweli kuwa kiungo huyo amekuwa katika kiwango bora msimu huu.”

AZAM FC YAWAPA TANO WACHEZAJI WAKE KUITWA STARS AZAM KUANZA MAZOEZI KESHO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply