kimataifa

POCHETTINO KURUDI TENA TOTTENHAM

admin May 30, 2021 12:48 pm


 TOTTENHAM imeanza mazungumzo na kocha wao wa zamani, Mauriccio Pochettino ili awe sehemu ya kumshawishi nyota wao Harry Kane ambaye anahitaji kusepa ndani ya kikosi hicho.

Pochettino alifundisha timu hiyo kuanzia mwaka 2014 hadi 2019 na alifukuzwa Novemba mwaka jana baada ya kuwa na msimu mbovu kisha akatua ndani ya PSG.

Kwa sasa inaelezwa kuwa hana furaha ndani ya PSG na taarifa zinaeleza kuwa Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy anataka kuanza mchakato wa kumrejesha tena.

Kocha huyo mwenye miaka 49 ameiongoza PSG kutwaa taji la French Super Cup na French Cup ila amekosa ubingwa wa Ligue 1 na timu yake ilitolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya na Manchester City katika nusu fainali.

SIMBA YAITAJA AZAM FC KUWA NJIA YAO KUFIKA FAINALI NYOTA WATATU SIMBA WAWANIA TUZO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply