Home Simba SC HIVI NDIVYO GOMES WA SIMBA ANAVYOFIKIRIA KUHUSU YANGA

HIVI NDIVYO GOMES WA SIMBA ANAVYOFIKIRIA KUHUSU YANGA


 HASIRA za Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes kwa sasa zipo katika kubeba makombe mawili ya ndani ambayo anashindania sambamba na watani zao wa jadi, Yanga.

 

Gomes amepania kumaliza msimu huu kwa kutetea mataji yao waliyoyatwaa msimu uliopita ambayo ni Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho la Azam.

 

Tayari ndani ya Ligi Kuu Bara, Simba ndiyo vinara wakiwa na pointi 61 baada ya kucheza mechi 25.


Mbio zao za kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika zilikwama Mei 22 baada ya kutolewa na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 4-3 ambayo Simba ilifunga.

 

 Gomes amesema: â€œKikubwa ni kuangalia namna ya kutetea mataji yetu msimu huu, haitakuwa rahisi kwetu kuona tunayapoteza na kwenda sehemu nyingine.

 

“Tutapambana kwa nguvu zote kutetea mataji yetu kwani malengo yetu ni kuona kwamba tunabeba mataji yote ambayo tutashiriki kwa sasa,”.


Msimu huu ikitokea Simba ikabeba tena mataji hayo, itakuwa ni msimu wa nne mfululizo Yanga inakosa ubingwa wa Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho la Azam.


SOMA NA HII  DENSA: TUTAANZIA TULIPOISHIA