Home Simba SC KIKOSI KAMILI CHA SIMBA SC DHIDI YA KAGERA SUGAR LEO

KIKOSI KAMILI CHA SIMBA SC DHIDI YA KAGERA SUGAR LEO

 


Kocha Mkuu, Didier Gomez na wasaidizi wake wamepanga kikosi kamili kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam hatua ya 16 bora dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa leo saa moja usiku.

Gomez amewaanzisha mlinda mlango namba moja Aishi Manula akisaidiwa na walinzi Shomari Kapombe, Mohamed Hussein, Joash Onyango na Pascal Wawa.

Katika eneo la kiungo wa ukabaji amewaanzisha Taddeo Lwanga na Jonas Mkude huku washambuliaju wakiwa ni Clatous Chama, Luis Miquissone na Rally Bwalya wakati idara ya ushambuliaji itaongozwa na Medie Kagere.

Baadhi ya wachezaji wanaoanzia benchi ni washambuliaji John Bocco, Chris Mugalu na kiungo mshambuliaji Bernard Morrison.

Kikosi Kamili kilichopangwa

1. Aishi Manula

2. Shomari Kapombe

3. Mohamed Hussein ©

4. Joash Onyango

5. Pascal Wawa

6. Taddeo Lwanga

7. Clatous Chama

8. Jonas Mkude

9. Medie Kagere

10. Rally Bwalya

11. Luis Miquissone

Wachezaji wa Akiba

Gk. Beno Kakolanya

02. David Kameta

03. Erasto Nyoni

04. Mzamiru Yassin

05. Chris Mugalu

06. John Bocco

07. Bernard Morrison

SOMA NA HII  EEHE...UMESIKIA ALICHOSEMA MUGALU HUKO SIMBA..?...AFUNGUKA A-Z YALIYOJIFICHA MOYONI...