Home Simba SC NYOTA WATATU SIMBA WAWANIA TUZO

NYOTA WATATU SIMBA WAWANIA TUZO


 NYOTA watatu wa kikosi cha Simba wameingia katika kinyang’anyiro cha kusaka mchezaji bora wa mwezi Mei.

Tuzo hiyo ni maalumu kwa ajili ya mashabiki kuweza kuchagua mchezaji ambaye wanaona anastahili kusepa na tuzo hiyo  kutokana na kile ambacho amekifanya katika mwezi husika.

Mchezaji wa kwanza kusepa na tuzo hiyo ambayo inadhaminiwa na Emirate Aluminium Profile alikuwa ni kiungo, Luis Miquissone na kwa mwezi Aprili ni Clatous Chama alisepa na tuzo hiyo.

Wachezaji ambao wanawania tuzo hiyo ni pamoja na John Bocco ambaye ni nahodha, Bernard Morrison ambaye ni kiungo na Taddeo Lwanga yeye ni mkata umeme.

SOMA NA HII  UKWELI MCHUNGU....KWA SIMBA HII YA 'WACHOVU' WENGI...HUENDA TAIFA LIKAPATWA NA AIBU KWENYE CAF SUPER LEAGUE..