Azam FC

WAKATI SIMBA NA YANGA ZIKIKIMBILIA MOROCCO, AZAM WAKIMBILIA HUKU KWA AJILI YA KAMBI

admin August 13, 2021 7:46 am


BAADA ya Simba na Yanga kutangaza kuweka kambi ya maandalizi ya msimu ujao nchini Morocco, wababe wenzao Azam wamewakwepa na kupanga kupiga kambi nchini Zambia katika jiji la Ndola.

Awali Azam walikuwa na mapendekezo mawili ya kambi ambapo walipanga kwenda nchi moja kati ya Afrika Kusini na Zambia na kuyachakata na hatimaye huenda siku za hivi karibuni wakasafiri kwenda Zambia sehemu ambayo aliipendekeza kocha mkuu wa timu hiyo, George Lwandamina.

Maandalizi hayo yamepangwa kuanza wiki ijayo kama mambo yataenda vizuri na timu tayari ipo kambini Chamazi, ikijifua tangu Jumatatu ya wiki hii ikisubiri taratibu za kwenda Zambia zikamilike.

Moja ya vigogo wa Azam alidokeza  kuwa wamefunga hesabu kwenye usajili wa wachezaji wa kimataifa na sasa wako kwenye harakati za kunasa nyota wasiozidi watatu wa ndani kisha kwenda Zambia.

“Usajili wa wachezaji wa kigeni tumemaliza, tumebakiza nafasi chache tu za wachezaji wa ndani ambao kwa sasa siwezi kuwataja,” alisema.

VIDEO:CHAMA AONDOKA SIMBA, DJUMA, MOLOKO WATUA DAR MSIMU MPYA, VIBE JIPYA NDANI YA EPL NA LALIGA WIKIENDI HII

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply