Azam FC

AZAM FC YAMTABULISHA JONAS TIBOROHA

admin August 16, 2021 10:43 am

 

UONGOZI wa  Azam FC, leo Agosti 16 umemtambulisha Mkurugenzi wa Masuala ya Mpira, Jonas Tiboroha ambaye atafanya kazi ndani ya timu hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, katika ukumbi wa mikutano ulipo Mzizima, Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdukarim Amin amesema kuwa malengo makubwa ya timu hiyo ni kuzidi kujiimarisha katika kila sekta ili kuwa imara zaidi.

Amin amesema:-“Kwa muda mrefu wengi wamekuwa wakimtambua CEO peke yake pamoja na watendaji wengine lakini leo tunamtambulisha kwenu Mkurugenzi wa Masuala ya Mpira.

“Kazi kubwa ni kuona namna gani tunaweza kuwa imara na kuzidi kuboresha timu yetu kwa sababu anakuja kufanya kazi katika kuyafikia malengo ambayo tumeweka,” amesema.

Tiboroha ambaye amepewa dili la mwaka mmoja amesema kuwa amekubali kufanya kazi hapo kwa kuwa ni moja ya timu bora na yenye mipango makini.

“Nimekubali kuja kufanya kazi hapa kwa kuwa ni moja ya timu bora, kazi ambayo nakuja kuifanya  ipo kwenye mpango kazi,” .


HALI YA HEWA MORROCO KWA SIMBA FRESH TU STRAIKA MPYA YANGA ASHTUA..FAMILIA YAKE WAFUNGUKA HAYA KUMUHUSU..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply