SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeingiamkataba wa haki ya matangazo ya Ligi Kuu kwa upande wa Radio na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wenye thamani ya Sh bilioni 3 wa muda wa miaka 10.
Ni leo Agosti 3 ambapo kulikuwa na shughuli za kusaini mkataba huo mpya na wenye makubaliano kwa pande zote mbili ambapo Rais wa TFF, Wallace Karia aliweza kumwaga wino kwa ajili ya mkataba huo.
Ni Gabriel Nderumaki, Mratibu wa Masuala ya Masoko alikuwa ni mmoja ya wale waliosaini mkataba huo kwa upande wa TBC.