Home news MANARA AENDELEA KUIKALIA KOONI SIMBA…AWALIPUA TENA KUHUSU JANJA JANJA ZAO…AMTAJA MWAMNYETO…

MANARA AENDELEA KUIKALIA KOONI SIMBA…AWALIPUA TENA KUHUSU JANJA JANJA ZAO…AMTAJA MWAMNYETO…


KLABU ya Yanga imedai kutotendewa haki na baadhi ya maamuzi yanayotolewa na waamuzi wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Bodi ya Ligi kwa ujumla kwani wamekuwa wakiegemea upande wa Klabu ya Simba pekee na si kwa vilabu vingine vya ligi hiyo.

Manara amesema hayo jana Jumanne, Faebruari 8, 2022 na Msemaji wa Klabu ya Yanga, Haji Manara wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam kuhusu mwenendo wa uendeshaji wa ligi hiyo inayoendelea.

“Utapaje Quality Players wa kisawasawa, utafuzu vipi AFCON back to back, utakwendaje World Cup kama Ligi unayotegemea uzalishe wachezaji wa Timu ya Taifa inakuwa na malalamiko ya maamuzi kila siku.

“Kuna matukio yasiyopungua 9 mpaka 10 yanayohusisha mechi za Simba ambazo watu wamelalamika kama watu wanavyolalamika kwenye mechi zingine hatuna shida na hilo lakini hiyo humanity iwe kwa timu zote.

“Maamuzi yawe sawa anayekosea aadhibiwe tu, wajibu wetu sisi ni kukumbusha hatulalamiki, hatuwezi kukubali kuona haki haitendeki alafu nikae kimya, tunataka haki itendeke

“Kuna mechi Simba waliomba kutocheza kwasababu wachezaji wao wanaumwa the next day sisi tunacheza Sumbawanga, hakuna mechi ngumu tuliyocheza kama ile ya Prisons wachezaji wameingia wanaumwa lakini tuliambiwa hamjafuata utaratibu jinsi ya kuomba, kina Mwamnyeto na mapanadol sita sita, mchezaji akitoka Half Time anakula Panadol anakula Diclopar.

“Mechi na Biashara, Beki wa Simba kafanya mchezo wa hatari kabisa, nani alichukuliwa hatua? Mechi mmoja Golikipa wao alifanya mambo ya ajabu kabisa lakini hakuchukuliwa hatua, unawezaje kuchukua hatua tukio la Polisi ukaacha tukio la Biashara,” amesema Haji Manara.

SOMA NA HII  SLOTI YA MEGA JADE KASINO USHINDI KWA NJIA 10.....