Habari za michezo

METACHA MNATA AZUA YA KUZUA ….POLISI TANZANIA WAIBUKA NA KUMNG’ANG’ANIA BAADA YA KUSAINI TIMU INGINE…

admin July 19, 2022 11:11 am


Siku chache baada ya Singida Big Stars (SBS) kumtangaza kipa Metacha Mnata kama mchezaji wao kwa ajili ya msimu wa 2022/23, Polisi Tanzania wameibuka na kuthibitisha kipa huyo ni mchezaji wao halali.

SBS imepanda daraja msimu huu na hadi sasa imesajili wachezaji sita kwa ajili ya kuongeza nguvu msimu ujao wa Ligi Kuu.

Akizungumza na Mwanaspoti, Makamu Mwenyekiti wa Polisi Tanzania, Robert Munis alisema Metacha ni mchezaji wao halali kwani bado ana mkataba wa mwaka mmoja na timu yao.

“Tumeshangazwa na taarifa za usajili wa Metacha na timu nyingine wakati wanafahamu ni mchezaji wetu halali kwasababu aliingia mkataba na sisi wa miaka miwili, ametumikia msimu mmoja bado mmoja,” alisema na kuongeza;

“Tunatarajia kuingia kambini kuanzia Agosti 17 hadi 20 ndani ya tarehe hizo tunatarajia pia kumwona Metacha akiungana na timu yetu kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi, hivyo sina mengi zaidi ya kuzungumza kwa sababu mkataba upo.”

Akizungumzia maandalizi ya msimu mpya alisema kwa sasa wanaendelea kufanya usajili na kuingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu.

Mkurugenzi wa ufundi wa SBS, Muhibu Kanu alifafanua juu ya mchezaji huyo waliyemsajili kuwa kwa mujibu wa mchezaji aliwathibitishia kuwa ni mchezaji huru ndio maana walifanya naye makubaliano.

“Tumesikia taarifa za Polisi Tanzania kuthibitisha kuwa bado wana mkataba na Metacha sio jambo jema walilolifanya kwenda moja kwa moja kwenye vyombo vya habari sheria zipo wazi wangefuata utaratibu,” alisema na kuongeza;

“Tunawaheshimu Polisi Tanzania kama kweli wana mkataba na Metacha tunawakaribisha mezani tulijadili hilo ili tusifike mbali zaidi na sio kufanya walichokifanya, jambo ambalo linaweza kutatuliwa kisheria au kulimaliza mezani sisi ni wamoja hatuwezi kugombea fito moja wakati tunalijenga soka letu lifike mbali,” alisema Kanu.

USAJILI WA MASTAA WAPYA SIMBA KUMTIA KWENYE MAJARIBU YA KWANZA KOCHA MAKI… BAADA YA KUANZA KUTUPIA SIMBA…OKRAH ATOA UJUMBE HUU KWA MASHABIKI NA KWA KOCHA MPYA….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply