Home Habari za michezo MSUVA AMALIZANA NA WAARBU WENGINE….MKATABA WAKE NI KUFRU NA NUSU…KULIPWA MILIONI 117...

MSUVA AMALIZANA NA WAARBU WENGINE….MKATABA WAKE NI KUFRU NA NUSU…KULIPWA MILIONI 117 KWA MWEZI…


Baada ya kusitisha mkataba na Mabingwa wa Afrika, Wydad Casablanca, Simon Msuva (28) amekamilisha mipango ya kujiunga na timu ya daraja la pili ya Al-Qadsiah ya Saudi Arabia.

Msuva amejiunga na klabu ya Al Qadsiah ya Saudi Arabia kwa mkataba wa mwaka mmoja utakaomfanya alipwe mshahara wa USD 500,000 kwa msimu sawa na Tsh Bilioni 1.7 sawa na kulipwa USD 50,000 (Tsh Milioni 117) kwa mwezi.

Aidha, mshambuliaji raia wa DR Congo, Walter Bwalya (27) amejiunga na klabu ya Al-Qadsiah ya Saudi Arabia kwa mkopo akitokea Al Ahly ya Misri

Bwalya anaungana na Msuva ambaye naye amesajiliwa na klabu hiyo ya ligi daraja la pili nchini humo.

SOMA NA HII  ZIMBWE JR AKUBALI KUPITIA NYAKATI NGUMU...KUMBE SIMBA WALICHUKUA MATAJI 5