MLINDA mlango wa Klabu ya soka ya Simba Aishi Manula amekanusha tetesi za kuongeza mkataba kwenye timu hiyo ambazo zimekuwa zikienea kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii.
Pia ameeleza kwamba anatamani kupata timu nyingine ambayo ataichezea na yuko huru kuichezea timu yoyote kwani hata uongozi wa klabu ya Simba ambayo anaichezea kwa sasa umesharidhia kuondoka kwake klabuni hapo na endapo kama atapata timu sahihi ya kuichezea basi klabu yake iko tayari kumruhusu bila pingamizi lolote.
Hata hivyo kwa siku za hivi kaibuni kulisambaa picha zikimuonyesha, Aish Manula akiwa sambamba na meneja wake Said Kazumary wakifuatii kile kilichoandikwa kwenye mkataba huo…