Home Habari za michezo PAMOJA NA SIMBA KUFUNGWA NA YANGA JUZI…AHMED ALLY AIBUKA NA KUJISIFU WALIVYOJAZA...

PAMOJA NA SIMBA KUFUNGWA NA YANGA JUZI…AHMED ALLY AIBUKA NA KUJISIFU WALIVYOJAZA UWANJA ..”TUMEYAONA MACHOZI”…


Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amewapoza mashabiki wa timu hiyo baada ya kufungwa bao 2-1 na watani wao wa jadi, Yanga, katika mechi ya Ngao ya Jamii iliyopigwa juzi Jumamosi, Agosti 13, 2022.

“Licha ya kuwa tulimaliza msimu bila taji lakini mechi ya ufunguzi wa ligi mashabiki wetu ndo walijaa zaidi kuliko wapinzani.

“Ni imani na mapenzi makubwa waliyonayo kwa timu yao, Imani na mapenzi ya mashabiki ni vitu vinapaswa kulindwa kabla havijapotea.

“Tumeyaona machozi ya kila Mwanasimba, tumesikia malalamiko ya kila Mwanasimba na tumepokea maoni yenu, hakuna chozi la Mwana Simba litapotea bure na hatuko tayari kuendelea kuwaumiza. Poleni tenaaa,” amesema Ahmed Ally.

SOMA NA HII  UJUMBE WA SIMBA KWA AS VITA YA DR CONGO