Home news TANZANIA YATOLEWA ‘USHAMBA’ KOMBE LA DUNIA WANAWAKE INDIA…

TANZANIA YATOLEWA ‘USHAMBA’ KOMBE LA DUNIA WANAWAKE INDIA…

0

Timu ya taifa ya wasichana U17 (Serengeti Girls) imeanza vibaya Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuchapwa mabao 4-0 na Japan katika mchezo wa Kundi D jana jioni Uwanja wa Jawaharlal Nehru (Fatorda Stadium) huko Margao, Goa nchini India.

Serengeti Girls itateremka tena dimba Jumamosi kumenyana na Ufaransa katika mechi wake wa pili wa Kundi D – kabla ya kukamilisha mechi zake za Kundi hilo kwa kumenyana na Canada Jumanne ijayo.