Habari za Yanga
Habari za michezo

MAYELE : SUDAN PALIKUWA PAGUMU SANA…LAZIMA TUFANYE JAMBO…

admin October 19, 2022 4:34 pm

Straika wa Yanga, Fiston Mayele amesema mazingira magumu waliyokutana nayo kwenye mchezo wa marudiano dhidi ya Al Hilal ya Sudan ndiyo yaliyochangia wao kupoteza mchezo huku viongozi wakisisitiza kuweka nguvu michezo yao ijayo ikiwemo mechi yao na watani, Simba itakayochezwa Oktoba 23, mwaka huu.

Yanga iliondolewa kwenye mashindano hayo kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 Dare es Salaam na kulala 1-0 katika marudiano.

Akizungumza mara baada ya kutua nchini wakitokea Sudan, Mayele alisema ugenini walikutana na mazingira magumu ambapo wapinzani wao walitumia vizuri uwanja wa nyumbani na kupata bao la mapema ikiwa ni tofauti na mechi iliyochezwa Kwa Mkapa.

“Wachezaji tumekutana na kufanya kikao kizito ikiwemo sisi wenyewe kuhimizana zaidi kila mmoja kufanya vizuri katika michezo iliyo mbele yetu na kusahau yaliyotokea huko Sudan,” alisema Mayele na kuongeza;

“Wachezaji kila mmoja ameonyesha kuumizwa na matokeo haya ila tunakusanya nguvu kwa pamoja kurudi na matokeo bora kwenye Kombe la Shirikisho Afrika pamoja na mashindano ya ndani.”

VIPERS WAITAMANI SIMBA LIGI YA MABINGWA AFRIKA…WATAMBA KUITOA ‘SHURUBU’…. BAADA YA KUBEBA TUZO YA Ballon D’Or JUZI…BENZEMA ATAJA TIMU ATAKAYOSTAAFIA SOKA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply