Habari za michezo
ALLY KAMWE :- TUMESHTUSHWA NA PROPAGANDA ZA SIMBA…KESHO WATAONA UBOVU WETU…
admin
October 22, 2022
7:16 pm
Afisa Habari wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe amesema kuwa siku ya Jumapili watakwenda kuwaonesha watani Simba kuwa wao sio wabovu kisa kufungwa na Al Hilal FC kunako Ligi ya Mabingwa Afrika.
”Tunakwenda kuwajibu Simba kwa vitendo, tumeshtushwa na propaganda za kusema kuwa Yanga ni mbovu. Sisi Klabu Bingwa Afrika tulishindwa kutimiza malengo yetu lakini haimaanishi sisi sio bora.”
Yanga inajipanga kukabiliana na Simba kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa siku ya Jumapili katika uwanja wa Benjamin Mkapa.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.