Kipa huyo aliyejiunga na Wajelajela hao katika dirisha dogo msimu uliopita akitokea Taifa Jang’ombe ya Zanzibar, anasema hatasahau ligi ya msimu uliopita kutokana na magumu aliyokutana nayo. Alicheza mechi 13 zikiwamo za Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) na kwamba haikuwa kazi rahisi kuinusuru timu hiyo ili kubaki Ligi Kuu.
Abel anasema baada ya kukosa namba Coastal Union alishauriwa na mchezaji mwenzake Adil Sultan kwenda kusaka maisha Zanzibar na kufanikiwa kupata Taifa Jang’ombe.
Mchezaji huyo anasema makipa wengi Ligi Kuu wanafanya vizuri na kwa viwango bora, lakini kwake Manula ni namba moja. “Kwa ujumla Manula namkubali sana. Siyo kwamba wengine hawafanyi vizuri la, ila huyu ni namba moja anajua sana. Hata hivyo natamani siku moja nicheze naye timu moja haijalishi Simba au kwingine,” anasema Abel.