Habari za michezo

ULAYA NI ULAYA TU….WAFANYAKAZI REAL MADRID WAPEWA NDINGA MPYAA…GARI MOJA BIL 3…

admin November 17, 2022 4:00 pm

Wachezaji na Wafanyakazi wote wa Real Madrid wamezawadiwa magari ya kifahari aina ya BMW.

Kama ilivyoripotiwa na Jarida la Daily Mail limesema kwamba kila mchezaji atapokea gari aina ya BMW lenye thamani ya kiasi cha Tsh. Bilioni 3.

Wachezaji na wafanyakazi wa Madrid wanaruhusiwa kuchagua gari kati ya matoleo ya iX na i4 na rangi yoyote watakayopenda.

Real Madrid awali ilikua na Mkataba na Kampuni ya kutengeneza magari ya Audi, lakini walishindwa kuelewana katika baadhi ya vipengele na kushindwa kuingia Mkataba mpya.

Dili la BMW linakadiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 6.5 kwa mwaka.

KAZE : YANGA KUWA ‘UNBEATEN’ NI FAIDA….KUNA WATU WANATUOGOPA AFRIKA NZIMA.. FT: YANGA SC 4-1 SINGIDA BIG STAR….MAYELE AFANYA YAKE…KAGERE AENDELEA KUWACHOVYA YANGA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply