Habari za michezo
BAADA YA KUFANANISHWA NA ‘PANYA’…ROONEY AJIBU MASHAMBULIZI KWA RONALDO…
admin
November 19, 2022
2:43 pm
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Wayne Rooney amefunguka na kumjibu Cristiano Ronaldo ambaye amemuita “panya” katika mahojiano yake na Piers Morgan.
Akijibu swali juu ya mahojiano hayo Rooney amesema:
“Sawa, sikiliza, Cristiano Ronaldo ni mchezaji mzuri na, kama nilivyosema hapo awali, yeye na Messi ndio wachezaji wawili bora zaidi kuwahi kucheza soka.”
“Na, nilichokisema sio ukosoaji. Nilichosema ni umri unakuja kwa kila mmoja wetu na Cristiano ni wazi anahisi sasa kwamba hatimaye anapaswa kukabiliana na hilo.”
Ronaldo akizungumzia jinsi wachezaji wenza wa zamani wanavyomkosoa akiwemo Rooney na Gary Neville.
Ronaldo alifichua kuwa haelewi kwanini wanamkosoa sana na kudai kuwa sio rafiki zake tena kabla ya kumwita Rooney ‘panya’.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.