Habari za Yanga SC
Habari za michezo

MCHEZO WA DAKIKA ZA KUSIMAMA WARUDI TENA YANGA…LEO ZAMU YA GSM…

admin November 22, 2022 1:21 pm

Leo Jumanne, Novemba 22, 2022, Yanga itashuka uwanja wa Liti mkoani Singida kuikabili Dodona Jiji kwenye mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Afisa habari wa Yanga Ally Kamwe amesema kesho katika mchezo huo watafanya matukio mawili makubwa.

Kwanza ni kuendeleza utaratibu wa kuwapongeza wachezaji na benchi la ufundi baada ya kucheza mechi 47 za ligi kuu bila kupoteza.

Tukio hilo litafanyika katika dakika 47 ya mchezo ambapo mashabiki wa Yanga watasimama kwa dakika moja kuwapigia makofi wachezaji pamoja na benchi la ufundi.

Lakini pia tukio hilo litakwenda sambamba na pongezi kwa Mfadhili/Mdhamin wa klabu ya Yanga Ghalib Said Mohammed ‘GSM’ ambaye juzi ilikuwa siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake.

Wananchi watatumia mechi dhidi ya Dodoma Jiji kumshukuru na kumtakia kila la kheri katika majukumu yake

GSM ndiye chachu ya furaha ya Wananchi kwa sasa, uwekezaji wake ndani ya klabu ya Yanga umekuja na mafanikio makubwa.

ILE SINEMA YA MPOLE NA MABOSI ZAKE…YAFIKIA HATUA HII…GEITA WAKIMBILIA INSTGRAM… KISA CHAMA… OKRAHA NA PHIRI WAAPA IPO SIKU TIMU MOJA ITAKIONA CHA MOTO..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply