Imeongeza kuwa mchakato huo utajumuisha tathmini ya mipango kadhaa ya kuimarisha klabu, ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa Uwanja, Miundombinu na upanuzi wa shughuli za Kibiashara za kilabu katika kiwango cha kimataifa, ili kuongeza mafanikio ya muda mrefu ya klabu hiyo kwa upande wa Timu za Wanaume, Wanawake na Vijana ili kuleta manufaa kwa Mashabiki na Wanachama wengine.
Familia ya Glazer pia inamiliki timu ya inayoshiriki Mchezo wa American Footbal ‘NFL’ ya Tampa Bay Buccaneers tangu mwaka 1995 na Avram Glazer alinunua timu katika ligi mpya ya kriketi ya Falme za Kiarabu ya Twenty20 mnamo 2021.
United walikuwa sehemu ya mradi wa Ligi Kuu ya Ulaya uliofeli ambao uliporomoka haraka Aprili 2021. Mwenyekiti mwenza wa Manchester United Joel Glazer baadaye aliomba radhi kwa machafuko yaliyosababishwa.