Habari za Simba leo
Habari za michezo

KISA YANGA….MANULA ‘AWACHANA LIVE’ MASTAA WENZAKE SIMBA…

admin December 17, 2022 10:35 am

Kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula amesema ili kulirudisha taji la Ligi Kuu msimu huu ni lazima wachezaji wajitoe kwa ajili ya timu.

Kipa huyo amesema wachezaji wenzake wa Simba ni lazima wacheze kwa bidii kutokana na ushindani uliopo kutoka Yanga na Azam.

Manula amemaliza mzunguko wa kwanza akiongoza kwa kutoruhusu bao mara sita katika michezo 11 aliyodaka kwenye mzunguko wa kwanza wa Ligi.

“Ligi ya msimu huu imezidi kuwa ngumu ndio maana nikasema mbali ya mbinu kutoka kwa benchi la ufundi lakini ni vyema kila mchezaji akatimiza wajibu wake ndani ya uwanja,” alisema Manula.

Kipa huyo amesema wajibu huo usiangalie kwenye ligi kuu peke yake bali hata mashindano ya kimataifa.

MKAKATI WA SIMBA KWA LIGI KUU TZ UKO HIVI….KAZI KUANZA RASMI KESHO…. NABI: TULIENI…HAO WAARABU TUNAPIGA KAMA KAWA…. WANATOKEA MTAANI KWANGU KABISA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply