Habari za Simba SC
Habari za michezo

BAADA YA KUCHEMSHWA NA ISHU YA CHAMA….KIGINGI KINGINE CHA MBRAZILI SIMBA HIKI HAPA…

admin January 21, 2023 4:44 pm

Kikosi cha Simba SC leo Jumamosi, Januari 21, 2023 asubuhi kimerejea tena mazoezini kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa Jumapili Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mbeya City wachezaji wa Simba walipewa mapumziko ya siku moja na kesho wachezaji watarejea mazoezini.

Wachezaji wapya waliosajiliwa katika dirisha hili Hamed Ismael Sawadogo, Jean Baleke na Mohamed Mussa watashiriki mazoezi hayo.

Inadaiwa kuwa Kama Kocha Mkuu Roberto Oliviera ‘Robertinho’ na wasaidizi wake wataona inafaa wanaweza kuwatumia katika mchezo huo kwa kuwa masuala yao ya vibali tayari yamekamilika.

WAKATI MASHABIKI ‘WAKIENJOY’….KUMBE NABI ‘KAVURUGWA’ NA USAJILI WA MUSONDA YANGA… KISA TABIA ZAO ZAKUFANANA…MORRISON, AZIZ KI WAPEWA KIBANO YANGA…ISHU IKO HIVI…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply