Habari za michezo
BAADA YA KUCHEMSHWA NA ISHU YA CHAMA….KIGINGI KINGINE CHA MBRAZILI SIMBA HIKI HAPA…
admin
January 21, 2023
4:44 pm
Kikosi cha Simba SC leo Jumamosi, Januari 21, 2023 asubuhi kimerejea tena mazoezini kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa Jumapili Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mbeya City wachezaji wa Simba walipewa mapumziko ya siku moja na kesho wachezaji watarejea mazoezini.
Wachezaji wapya waliosajiliwa katika dirisha hili Hamed Ismael Sawadogo, Jean Baleke na Mohamed Mussa watashiriki mazoezi hayo.
Inadaiwa kuwa Kama Kocha Mkuu Roberto Oliviera ‘Robertinho’ na wasaidizi wake wataona inafaa wanaweza kuwatumia katika mchezo huo kwa kuwa masuala yao ya vibali tayari yamekamilika.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.