Habari za Yanga
Habari za michezo

HAWA HAPA MASTAA MUHIMU WA YANGA WATAKAOKOSEKANA MECHI NA MAZEMBE…DIARRA NDANI…

admin March 25, 2023 5:59 pm

Kumekuwa na stori nyingi kwenye mitandao ya kijamii kuwa Yanga itawakosa wachezaji wake wengi kwenye mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe nchini Congo.

Hii inatokana na kile kinachoelezwa kuwa ni kutokana na kupata kadi mbili za njano katika michezo miwili inayofuatana ya michuano hiyo.

Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya CAF, mchezaji atakosa mchezo unaofuata kwa kupata kadi mbili za njano mfululizo.

Kwa Yanga Djuma Shabani pekee ndiye aliepata kadi mbili za njano katika mechi mbili zilizofuatana, alipata kadi katika mechi ya Real Bamako katika Dimba la Mkapa na mchezo dhidi ya Us Monastir.

Mchezaji mwingine aliyepata kadi ya njano katika mchezo wa Bamako ni mshambuliaji Kennedy Musonda ambaye mchezo wa pili hakupata kadi.

Lakini katika mchezo wa wikiendi iliyopita kati ya Yanga na Maonastir, wachezaji wa Yanga waliopata kadi ni wanne.

-Djigui Diarra -Djuma Shabani -Ibrahim Bacca -Khalid Aucho

Kwa hiyo kwa kigezo cha adhabu ya kadi ni Djuma Shabani pekee vinginevyo kocha atakua ameamua kuwapumzisha nyota wake.

Au kocha atawapumzisha Djigui Diarra, Khalid Aucho na Ibrahim Bacca dhidi ya Mazembe kwa kuhofia wasije wakapata kadi ya pili itayowafanya wakose mechi ya robo fainali.

KOSA KOSA ZA KIBU ZIBUA JIPYA SIMBA…MBRAZILI ASHIDWA KUMVUMILIA..AMPA MAKAVU YAKE… KUHUSU MIQUISSONE NA AL AHLY …SAFARI HII….SIMBA WASHINDWE WENYEWE TENA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply