Habari za Simba leo
Azam FC

KOCHA AZAM FC AWATEMEA MBOVU WACHEZAJI…AMEZUNGUMZA HAYA

Marce Ben Komba April 10, 2023 12:21 pm

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Kally Ongala ameichifua kuwa, kwenye timu hiyo hakuna supastaa na mchezaji yeyeote anaweza kuanzia benchi na bado timu ikapata ushindi kama kawaida.

Kauli ya Ongala imejiri baada ya kuwaweka baadhi ya wachezaji wa timu hiyo benchi juzi usiku wakati Azam ikiizamisha tena Mtibwa Sugar kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara iliyopigwa Azam Complex, akiwemo Prince Dube na Kipre Junior ambao ni tegemeo wa kikiosi hicho.

“Unapokuwa na wimbi la wachezaji wengi bora unaamua leo aanze huyu na kesho yule kwa sababu hawatofautiani sana na hilo ndilo ambalo sisi kama benchi la ufundi tulikuwa tunalihitaji kutokana na kushiriki mashindano mengi.”

Ongala aliongeza mwenendo wa timu kwa sasa ni mzuri ingawa bado wana kazi kubwa ya kufanya ili wasitetereke kwani malengo yao ni kumaliza nafasi tatu za juu licha ya washindani wao Singida Big Stars kutishia nafasi hiyo.

Katika mchezo huo uliopigwa kuanzia saa 3:30 usiku, Azam ilishinda mabao 2-1 yaliyofungwa na Isah Ndala na Idd Seleman ‘Nado’, huku bao la kufutia machozi la Mtibwa likifungwa na Onesmo Mayaya.

Ushindi huo kwa Azam ni wa pili mfululizo dhidi ya Mtibwa kwani kabla ya hapo iliwafunga mabao 2-0 na kuitoa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) katika hatua ya robo fainali iliyochezwa Aprili 3 na kwenda nusu fainali na sasa itavaana na Simba kwenye hatu

BAADA YA KUONA MAFANIKO YA CAF YAMEKUJA….SENZO ARUDI UPYA YANGA…AMTONYA HAYA INJINIA HERSI… BEKI WYDAD CASABLANCA AWAOGOPA SIMBA…AVUNJA UKIMYA…ISHU NZIMA IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply