HAJI MANARA AUMBUKA...NI BAADA YA KUMGOMBANISHA RAISI YANGA NA MTANGAZAJI
Habari za michezo

HAJI MANARA AUMBUKA…NI BAADA YA KUMGOMBANISHA RAISI YANGA NA MTANGAZAJI

Marce Ben Komba April 12, 2023 8:46 am

Taarifa zisizothibitishwa zimeenea mitandaoni kuhusu Mchambuzi wa masuala ya michezo nchini kutoka Kituo cha televisheni cha Channel Ten, Juma Ayo kuwa alimuomba pesa Rais wa Yanga, Eng. Hersi Said ili akamtibie ndugu yake.

Taarifa hizo zilizochapishwa na na Msemaji wa Yanga, Haji Manara zinaeleza kuwa Hersi alimnyima pesa kijana huyo ndio maana yeye na wachambuzi wenzake wana chuki na Yanga na kufanya wazue taarifa za uongo kuhusu Yanga mara kwa mara.

Juma Ayo ameibuka na kujibu shutuma hizo akisema; “Kwa heshima ya klabu ya Yanga na viongozi wake niseme tu hakuna mazungumzo yangu na Engineer kumuomba pesa.

“Nitaendelea kutunza mazungumzo mbalimbali nayofanya na viongozi wa mpira kwa lengo la kudumisha amani na uadilifu.

“Tujikite kwenye football tuachane na personalities. Tuendelee kuzungumzia mpira na si mambo binafsi ya watu,” amesema Juma Ayo.

KIBADENI AWACHANA MASTAA WAZAWA SIMBA…”HAMFUNGI MNAJUA KUSHANGILIA TU KOCHA SIMBA SC AWAPUUZA WYDAD CA…”NAWAJUA HAWASUMBUI…AMEZUNGUMZA HAYA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply