Habari za Yanga
Habari za michezo

KIPIGO CHA YANGA CHAZUA VITA MPYA MJINI…JEMEDARI AMPIGA ‘DONGO’ LA MWAKA MANARA…

admin April 18, 2023 7:30 am

Baada ya Yanga kupokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Simba katika mchezo wa Dabi ya Kariakoo.

Jemedari Said amemtupia kijembe aliekuwa msemaji wa Yanga Haji Manara ambae aliwahi kutamba huko nyuma kwamba ataweza kufungwa na Yanga.

Kupitia Ukurasa wake wa Instagram Jemedari ameweka Video Clip ya Manara na kuandika;

“Kuna wakati tunaamini wajinga kwenye mambo ya msingi mpaka wanajiona “miungu watu”, ishatokea sasa inakuaje?

Mpira unataka heshima, derby inataka heshima. Mzee Kaduguda aliwahi kusema huwezi kuwafunga Yanga kama hauwaheshimu, manake Yanga wanaweza wakaokotana wazee kama yeye 11 wakaingia kiwanjani wakaifunga Simba.

Huyo ni mwandishi wa habari mkongwe nchini, Katibu Mkuu wa zamani wa FAT (sasa TFF), Mwenyekiti wa zamani wa Simba SC na mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu hiyo, Mwenyekiti wa zamani wa Ghymkhana club Dar es Salaam na msomi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam anaonyeaha kuheshimu mpira na miiko yake, halafu mjinga mmoja anasema yeye hawezi kufungwa mpaka anakufa na watu wanashangilia na kuamini, ndo nchi yetu sasa tufanyeje? Tunapawa kuachana na wadananda hawa hawajui boli wanaganga matumbo yao tu”.

MANGUNGU:- TUTAWAFUNGA YANGA MPAKA SIKU NAONDOKA SIMBA…. ILE SIKU YA USIKU WA ULAYA NI LEO….KAMATA ODDS ZA KIBABE KUTOKA MERIDIANBET KWA MSHIKO WA KUSHIBA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply