Home Habari za michezo BAADA YA KUWA KIMYA MUDA MREFU….OKRAH AANZA KUKINUKISHA SIMBA….JAMBO LAKE LA KWANZA...

BAADA YA KUWA KIMYA MUDA MREFU….OKRAH AANZA KUKINUKISHA SIMBA….JAMBO LAKE LA KWANZA HILI HAPA…

Habari za Simba

Klabu ya Simba imethibitisha kurejea kikosini kwa kiungo mshambuliaji Augustine Okrah ambaye alikuwa nje kwa zaidi ya wiki nne baada ya kuvunjika kidole

Taarifa iliyotolewa na Simba, imebainisha kuwa leo Okrah ameshiriki mazoezi na wachezaji wengine kikamilifu

Aidha winga Kibu Denis nae afya yake imeimarika leo amejumuika na wenzake katika mazoezi

Kibu na Shomari Kapombe waliumia kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca uliopigwa Jumamosi iliyopita

Simba imeingia kambini kujiandaa na mchezo wa robo fainali kombe la FA dhidi ya Ihefu Fc ambao utapigwa Ijumaa, April 07 katika uwanja wa Uhuru

SOMA NA HII  BAADA YA TETESI ZA KUACHANA NA SIMBA KUZAGAA JUZI NA JANA...BARBARA AVUNJA UKIMYA...ADAI CHANGAMOTO NI...