Habari za Yanga SC
Habari za michezo

MASHUSHU WA CAF WAVAMIA HOTEL YA YANGA…WATOA ‘DATA’ ZA WASAZUI NA TAHADHARI…

admin May 17, 2023 12:26 pm

Wakati wachezaji wa Yanga wakimalizia kula chakula cha mchana katika hoteli waliyofikia hapa Rustenburg, Afrika Kusini na viongozi wengine wakiendelea na shughuli za kitimu, ghafla waliingia Maofisa wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), ambao hawakutoa taarifa kabla.

Viongozi hao walikuwa watatu mmoja akiwa amevalia fulana yenye nembo ya CAF na wengine nguo za kawaida na kuingia moja kwa moja hotelini.

Walipoingia mlangoni walikutana na Meneja wa Yanga, Walter Harrison na ofisa wa ulinzi wa timu hiyo maarufu Penta na kuanza kuzungumza.

Mazungumzo ya viongozi hao wa CAF na wale wa Yanga yalidumu kwa muda usiozidi dakika 10 kisha kuondoka.

Inaelezwa viongozi hao walifika kambini hapo kuangalia usalama wa timu na kutoa baadhi ya maelekezo kuhusu mambo yanayohusu mchezo wa Marumo Gallants na Yanga.

Ikumbukwe leo saa 1:00 usiku za Tanzania na 12:00 jioni za hapa Afrika Kusini, Marumo wataikaribisha Yanga uwanjani kwenye mchezo wa pili nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga inahitaji ushindi au sare ya aina yeyote kwenye mechi hiyo ili kutinga fainali kwani ilishinda 2-0, nyumbani Tanzania kwenye mechi ya duru ya kwanza.

MAGAZETI SAUZI YAUZA NA STORI ZA YANGA TU….TIMU WENYEJI WAPEWA ‘ODDS’ NDOGO… MANULA, KAPOMBE WAIBUA JAMBO AZAM FC…MABOSI WAANZA ‘KUCHANGA KARATA UPYA”…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply