Habari za Michezo leo
Habari za michezo

AHMED ALLY :- YANGA WANANYANYASA WACHEZAJI WAO…WANAHELA ZA KULIPA WASANII TU…

admin June 15, 2023 1:09 pm

Wakati taarifa zikizagaa kuwa Wachezaji wa Yanga Princes (hasa wazawa) wamepanga kufanya maandamano ili kuushinikiza malipo yao baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya Wanawake.

Meneja wa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika andiko akionekana kama anawapa mbinu wachezaji hao namna ya kupata maslahi yao.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ahmed ameaandika;

Hela za kununua Wasanii si mngewalipa hawa Watoto wa kike?

Kwanini mnawanyanyasa sana? Kwa sababu hawana sauti ndo maana mnawadhalilisha?

Mmewatekelekeza kambini tangu ligi imemalizika May 17 wanaishi hovyo tuu

Mnafanya mambo mengi ya maigizo ili muonekane wasafi kumbe mnanyanyasa wadada wa watu

Misaada mnayotoa si mgeanza kwa kulipa haki za hawa Wadada?

Nimelia sana sijalala usiku kucha baada ya kuona hii taarifa

Poleni UTO Princess halafu msiende Jangwani na nyie pale kuna wauza jezi tuu nendeni Posta ndo mtawakuta”

Wachezaji wa Yanga Princess wanadaiwa kudai stahiki zao ikiwemo mishahara na pesa za usajili kwa baadhi ya wachezaji ambazo hawajalipwa mpaka hivi sasa.

IFANYE SIKU YAKO KUWA YA BAHATI NA CASINO HII YA MERIDIANBET… BREAKING NEWS: NDOA YA SIMBA NA VUNJA BEI YAISHA….ATAKAYEZALISHA JEZI MPYA HUYU HAPA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply