bangala
Habari za michezo

RASMI YANGA WAMUUZA BANGALA AFUATA NYAYO ZA FEI TOTO….. ATUA HAPA MAPOKEZI YAKE SASA

Staff Desk July 29, 2023 2:29 pm

KLABU ya Yanga imetangaza kumuuza mchezaji wake Yannick Bangala katika timu ya Azam.

Bangala hakuwemo kwenye utambulisho wa wachezaji katika kilelele cha Wiki ya Mwananchi Julai 22, 2023 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

“Uongozi wa Young Africans SC unapenda kuutarifu Umma kuwa tumefikia makubaliano na Klabu ya Azam FC kumnunua mchezaji wetu Yannick Bangala,” imesema Yanga kupitia mitandao yake ya kijamii.

yanick bangala

Katika taarifa yake Azam imesema:”Tumefikia makubaliano na klabu ya Yanga ya kumnunua, mchezaji kiraka, @ybangala4 na amesaini mkataba wa miaka miwili baada ya kufuzu vipimo vya afya.”

Bangala anakuwa mchezaji wa pili Yanga kumuuza Azam katika siku za hivi karibuni baada ya Feisal Salum kusaini kuwatumikia matajiri hao wa Chamazi Juni 8 mwaka huu.

SIMBA YAWEKA WAZI ISHU YA KUACHANA NA BANDA……. ISHU IKO HIVI WAWAKILISHI WA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA, SIMBA, YANGA, AZAM, SINGIDA FG, RATIBA KAMILI IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply