Habari za michezo
GAMONDI AWAGOMEA MABOSI WA YANGA, MECHI DHIDI YA AS VITA, SASA YANGA KUKIPIGA NA TIMU HII
Staff Desk
August 3, 2023
6:57 pm
Kama kuna kitu ambacho Gamondi amewashtua mabosi wake ni uamuzi wake wa kugomea mechi ambayo mabosi wake walitaka timu hiyo ikipige dhidi ya AS Vita ya DR Congo Jumapili, lakini akawaambia hakuna mchezo huo, labda upigwe Avic na hakuna shabiki kuingia.
Vita wako hapa nchini lakini Gamondi amegomea wao kucheza Chamazi na Yanga. Gamondi amewaambia mabosi wa Yanga kwamba atafutiwe mechi nyingine kwa timu ya ndani kisha wakipige kambini na sio Chamazi kwa kuwa atakuwa amekwenda kuuza silaha wakati Ngao ya Jamii ni wiki ijayo.
Tayari mabosi wa Yanga wameshachukua maelekezo hayo ambapo soka la bongo Inafahamu huenda JKU wakashuka mjini kutoka Unguja Zanzibar kuja kujipima na mabingwa hao, na Jumapili hakutakuwa na mechi kama ilivyotangazwa awali.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.