Habari za michezo
Habari za michezo

SIMBA, YANGA ZAIGANA MATOKEO MECHI ZA MAZOEZI….

admin September 10, 2023 1:23 pm

Wakongwe Yanga na Simba zimegawa dozi nzito kwenye mechi zao za kirafiki baada ya kushinda mabao 6-0 kila mmoja wakiendelea kujipima.

Tuanze na Simba ambao wakicheza kwenye Uwanja wao wa mazoezi pale MO Simba wamejipima dhidi ya Ngome na kufanikiwa kushinda kwa mabao 6-0.

Mabao ya Simba kwenye mchezo huo yamefungwa na mshambuliaji Jean Baleke aliyefunga mara mbili,Aubin Kramo, Willy Onana,Shomari Kapombe na Shaban Idd Chilunda.

Huo unakuwa mchezo wa tatu wa kirafiki kwa Simba tangu ligi isimame kupisha mechi za Kimataifa kwa Kalenda ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ambapo tayari walishazichapa Kipanga (3-0) kisha wakawachapa CosmoPolitan (5-1).

Yanga  wakacheza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Kiluvya United wakishinda kwa mabao 6-0 mchezo ukipigwa pale Uwanja wao wa mazoezi AVIC Town.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Crispin Ngushi, Farid Mussa huku Hafidh Konkoni, Kennedy Musonda wote wakifunga mara mbili kila mmoja.

VIONGOZI WA YANGA WATANGAZA KUFANYA KUFURU HII YANGA YASHUSHA CHUMA KINGINE SIO POA, JOB, MWAMNYETO MATATANI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply