Habari za Simba SC
Habari za michezo

ROBERTINHO AKOMAA NA KIKOSI CHA SIMBA AZIDISHA DOZI

Staff Desk September 10, 2023 11:43 am

ROBERTO Oliveira ‘Robertinho’ Kocha Mkuu wa Simba, ameweka wazi kuwa, kinachotakiwa kufanyika kwa sasa ni wachezaji wote kuongeza kasi na umakini wawapo ndani ya eneo la 18.

Timu hiyo ipo katika maandalizi ya mechi za kitaifa na kimataifa kwa msimu wa 2023/24, pia inapambana kutwaa taji la Ligi Kuu Bara.

Mazoezi ya Simba yanafanyika Simba Mo Arena ikiwa ni program zinazoandaliwa na benchi la ufundi la timu hiyo iliyo nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu Bara.

Robertinho amesema: “Kila wakati tunafanyia kazi makosa yaliyopita ili kuwa imara na tunatambua kwamba katika kufikia malengo ni muhimu kufanya yote kwa umakini.

“Kuanzia safu ya ushambuliaji na ulinzi kote ni muhimu kufanya kazi kwa umakini katika kutafuata matokeo chanya uwanjani na inawezekana.”

HUKO SIMBA KUNA VITA MPYA KUFA KUFAANA KUTOKA KMC MPAKA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply