KIPA CHIPUKIZI SIMBA AMWAGA SIRI NZITO...AMTAJA AISHI MANULA...ISHU IKO HIVI A-Z
Habari za michezo

AKILI YA SIMBA SASA NI KWA COASTAL UNION, MSUTUPANGIE KIPA LANGONI

Staff Desk September 19, 2023 10:43 am

Kikosi cha timu ya Simba kimerejea nchini jana Jumatatu, Septemba 18, 2023 wakitokea nchini zambia ambako walikwenda kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Power Dynamos ambapo walitoa sare ya bao 2-2.

Akizungumza leo, Meneja wa Habari na mawasiliano wa Kalbu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa kikosi hicho kimeelekea kambini moja kwa moja kwa ajili ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Coastal Union utakaopigwa keshokutwa Alhamisi, Septemba 21, jijini Dar es Salaam.

“Coastal Union tunawakaribisha, tulikuwa na hamu nao kweli tangu tulivyoomba tucheze mechi na wao kama wiki mbili zimepita, mambo yakawa mengi, mara wamevunja kambi.

“Kifupi ni kwamba walikula nyoya, lakini sisi ni people, tumekutana, Alhamisi tutakutana nao kwa ajili ya kwenda kuwapelekea moto Wagosi wa Kaya.

“Kuhusu kipa Ayoub Lakred, Coastal wasitupangie, anaweza akadaka kipa yeyote yule ambaye Simba SC tutamuamini,” amesema Ahmed Ally.

MWENYE NAMBA AMERUDI, AISUBIRI TIMU KAMBINI, MASTAA WAPEWA MAAGIZO MANARA ATUA MAKKAH, AWAOMBA WATANZANIA JAMBO HILI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply