Habari za Yanga SC
Habari za michezo

SIRI YA ‘MGOLI WA CAF’ ALIOFUNGA MZIZE YAANIKWA WAZI…MCHAKATO WOTE KUMBE ULIANZA HAPA..

admin October 3, 2023 4:54 pm

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Clament Mzize amefichua siri ya bao lake lililowapeleka makundi lilitokana na maelekezo kutoka kwa kocha Miguel Angel Gamondi aliyemtaka kutumia vizuri mipira ya krosi kwa ajili ya kupachika bao na kupata ushindi.

Bao la dakika 66 lililofungwa na Mzize ndio lililowapeleka Yanga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuiondoa Al Merrikh ya Sudan kwa jumla ya mabao 3-0 katika michezo yote miwili.

Nyota huyo alianzia benchi akichukuwa nafasi ya Kennedy Musonda na kufanikiwa kufunga bao pekee baada ya kuunganisha mpira wa krosi iliyopigwa na Joyce Lomalisa.

Mzize alisema akiwa katika bencho kocha (Gamond) alinipa maelekezo kuwa nikatumia vizuri mipira ya krosi na nafasi wazotengeneza ili kutafuta bao.

Alisema alienda kufanya maelekezoo aliyopewa na kufunga bao pekee ambalo amepokea krosi kutoka kwa Lomalisa na kufanya kile alichoambiwa na Gamondi.

“Aliniambia niwe makini na kutofanya makosa kwenye eneo la hatari na kutumia vizuri mipira ya krosi na nilifanikiwa kuipeleka timu hatua ya makundi.

Kuhusu kushangilia staili ya kutetema ambayo alikuwa akifanya Mayele (Fiston) kwa kuwa bado anaishi moyoni mwangu, alikuwa mtu wa kunipa moyo na hadI sasa tumekuwa tukiwasiliana na kunipa maneno ya kuweza kupambana katika hatua yangu ya uchezaji, “ alisema Mzize.

Alisisitiza kuwa hawataishia hapo hatua ya makundi kwa sababu wanahitaji kufanya vizuri katika kila mashindano na anaimani wataenda kucheza robo fainali ya Afrika kwa mwaka huu.

SIMBA WAOMBA ‘POO’ BODI YA LIGI….MBRAZILI AMTAJA BOCCO CAF… MPE PSG, MAN CITY NA NAPOLI LEO UIBUKE NA MTONYO WA UHAKIKA…MKEKA OG HUU HAPA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply