Habari za Simba SC
Habari za michezo

KIONGOZI WA YANGA AFUNGUKA KUHUSU KUMFUKUZA ROBERTINHO

Staff Desk October 11, 2023 4:19 pm

Makamu Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela amesema kama angekuwa kiongozi wa Simba SC basi tayari angekuwa amemtimu kocha wa Simba Robertinho kwasababu ni mchekeshaji (Comedy).

Akizungumza kupitia bongo5 Mwakalebela amekiri kuwa Simba SC ipo vizuri na ina wachezaji wazuri lakini tatizo la Wekundu hao wa Msimbazi ni benchi la ufundi (technical bench)

Mwakalebela amegusia suala la Mwamuzi akidai haelewi “kama wanakulaga (Simba) mayai na waamuzi sijui lakini kuna fairness fulani wanakosa. Marefarii sijui wana tatizo gani, nashindwa kuelewa kwanini kwenye mechi za Simba tu”

Aidha Makamu Mwenyekiti huyo wa zamani wa Yanga amesema haoni nafasi ya Simba kufika nusu fainali wala robo ya CAF Champions League kama Aish Manula hatokaa golini.

MARAIS HAWA KUISHUHUDIA SIMBA VS AL AHLY UONGOZI WA SIMBA UMEFUNGUKA HAYA KUHUSU WACHEZAJI WAKE WALIOITWA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply