Habari za Simba SC
Habari za michezo

KWELI HII HATARI WATU WANAIJUA SIMBA KULIKO STARS

Staff Desk October 16, 2023 4:42 pm

Mchambuzi wa soka Bongo, Amri Kiemba amechambua kuhusu mashabiki wa soka kuizungumzia klabu ya Simba kuliko timu ya Taifa.

Huu hapa uchambuzi wake;

“Inawezekana TFF ina lengo zuri la kuifanya Taifa Stars kuwa mbali na vyombo vya habari pamoja na mashabiki wa soka lakini kuna siku watawahitaji watu uwanjani na hapo TFF italazimika kutumia nguvu nyingi kuwashawishi.

Mwaka 2027 tutakuwa wenyeji wa AFCON, tunahitaji watu. Kama watu hawapo nyuma ya timu yao muda wote ikifika wakati wa AFCON ndio tuanze kuhimizana kwenda uwanjani kwa sababu sisi ndio wenyeji tutakuwa tumechelewa.

Kwa sasa watu wanafahamu sana kuhusu mechi ya Simba vs Al Ahly [African Football League] ambayo itachezwa Ijumaa lakini hawajui kitu kuhusu mechi ya Taifa Stars ambayo imechezwa jana!”

Ile mijadala ya kwa nini fulani ameitwa halafu fulani hajaitwa ndio inaongeza ufuatiliaji wa timu ya Taifa. Kila kitu kina chanya na hasi, hata hii kuita timu hadi inacheza kimyakimya nayo ina hasi na chanya.

GAMONDI ATOA ONYO KUHUSU UBINAFSI KISA MASTAA HAWA WAZIRI WA UTAMADUNI AWEKA UTABIRI WA KIBABE SIMBA, YANGA CAFCL

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply