Habari za Simba na Yanga
Habari za michezo

KUELEKEA MECHI YA KESHO SIMBA vs AL AHLY…JEMEDARI SAID ATUPA KOMBORA HILI KWA YANGA…

admin October 19, 2023 3:20 pm

Mchambuzi wa masuala ya soka nchini, Jemedari Said Bin Kazumari amesema kuwa Klabu ya Simba imewaacha mbali wapinzani wao Yanga SC kwenye soka la Kimataifa.

Jemedari amesema hayo kuelekea mchezo wa kesho wa African Football League kati ya Simba na AL Ahly, yakiwa ni mashindano mapya ya CAF huku Simba ikitarajiwa kuandika historia ya kuwa timu ya kwanza nchini Tanzania kushiriki michuano hiyo.

“Kwani unadhani Yanga walivyoingia fainali Simba walifurahia. Hata wao hawawezi kufurahia Simba kucheza African Football League na kwa kuwa hawana imani kama Al-Ahly anaweza kushinda dhidi ya Simba hawawezi kwenda uwanjani.

“Zamani walikuwa wanaenda kwa sababu walikuwa na uhakika Simba itafungwa. Kama Ahmed Ally anavyosema mwakani hadi IHEFU watashiriki African Football League, aliyeanza kaanza tu.

“Acheni kufichaficha, Simba ndio imefanya Tanzania iogopwe, waarabu zamani walikuwa wakipangwa na timu za Tanzania wanashangilia lakini kwa sasa hawataki kabisa yote Simba ndio kasababisha.

“(Yanga) Wanasema wamewaacha mbali, mbali hiyo wapi, maana inategemea na unatoka wapi. Simba imewaacha mbali sana kimataifa,” amesema Jemedari Saidi.

HUYU BWANA KAMA ANATAKA KUFANIKIWA BASI AONDOKE YANGA MISHAHARA YA WACHEZAJI YANGA KULIPWA MASTAA SIMBA WAKISHINDA KESHO…MO DEWJI AFANYA KUFRU…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply