HAJI MANARA AUMBUKA...NI BAADA YA KUMGOMBANISHA RAISI YANGA NA MTANGAZAJI
Habari za michezo

UHALISIA WA MANARA NA SOKA LA TANZANIA

Staff Desk October 20, 2023 1:54 pm

Simba na Yanga walikuwa na Hajis Manara lakini kwa sasa anatumikia adhabu ya kifungo alichopewa na Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania “TFF”.

Mtu akiniuliza swali; “Namjua vipi HAJI MANARA nje ya kazi alizowahi kufanya kama Afisa Habari?”, nitamjibu kirahisi sana “NAMFAHAMU @hajismanara KAMA GOOGLE YA MPIRA WA TANZANIA na Ulimwengu kwa Ujumla”.

Inawezekana ikawa vigumu watu kuniamini, Yes Sijawahi kukutana nae, Kukaa wala kuongea na Manara lakini nasoma na kumsikiliza sana ni kweli naweza kumtumia kama google ya mpira wa Tanzania kama navyomtumia Pascal Kabombe kwenye baadhi ya mambo.

Manara ndio kachora mchongo mzima kuhusu kujaza viwanja, Zakazakazi nisaidie kama miaka ya nyuma kuna Afisa Habari aliwahi kuita mashabiki uwanjani na wakajaa (Full House)

Hajis Manara alikuwa ni mwanadamu wa tofauti sana alipokuwa akisisimama mbele ya Camera kuongelea mpira basi hata kama ulikuwa unafanya shughuli zako ilikuwa rahisi sana kuziacha, Katika ubunifu na namna ya kuyaendesha matamasha makubwa Haji amekuwa ni mtu hasa.

Kwa kiasi kikubwa Maafisa Habari wa sasa wa vilabu kama Simba na Yanga wanafanya vyema lakini njia na kodi zote Manara ndio alifungua, ukijaribu kukumbuka kuhusu “Do or Die” ya kwa Mkapa, “The Return of Champion”, “War in Dar” n.k. zilikuwa ni juhudi kubwa sana za Manara.

SIMBA YATOA AHADI HII MECHI YA LEO AFL MWAKINYO AFANYA HAYA KWENYE ADHABU YA MANARA TFF

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply