Habari za michezo

DUKE ABUYA AIPIGA MKWARA YANGA

Staff Desk October 27, 2023 8:28 am

Nyota wa Singida Big Stars, Duke Abuya amesema ni muda kwao wa kuonyesha ubora wao mbele ya Yanga kesho kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

“Kila mchezo ni mgumu kama iliyopita na sisi wachezaji jukumu letu ni kuhakikisha tunapambana kwa ajili ya timu, hii ni nafasi nyingine ya kuonyesha ukubwa tuliokuwa nao kwa sababu uwezo na uzoefu tunao wa kukabiliana na yeyote,” alisema.

Duke aliyesajiliwa akitokea Police FC ya Kenya aliongeza ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Namungo katika mchezo uliopita, umewaongezea morali kubwa huku akianisha licha tu ya kuiheshimu Yanga kutokana na ubora wao ila hawatoingia kinyonge.

“Tunaiheshimu Yanga ila hatotakuja kinyonge kwani tunahitaji kupata pointi tatu pia,” alisema. Singida tangu imepanda haijawahi kuifunga Yanga

UONGOZI YANGA WAKAA KIKAO AJENDA KUU NI UBINGWA TU YANGA SASA WAWATAMANI AL AHLY BAADA YA SIMBA KUSHINDWA KUTAMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply